Katika kuadhimisha siku ya moyo Duniani tarehe 29/09/2018 Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) wafanya upimaji na utoaji wa elimu ya afya ya moyo bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni iliyopo wilaya ya Kigamboni.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndungulile akimsikiliza mkazi wa Kigamboni aliyejitokeza kupima magonjwa ya  moyo pamoja na kupata elimu ya afya bora ya moyo wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani ambapo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni iliyopo wilaya ya Kigamboni. Jumla ya watu 300 walipimwa afya zao ambapo 16 walikutwa na matatizo ya moyo ambayo yalihitaji matibabu ya kibingwa na kupewa rufaa ya kwenda kutibiwa JKCI.

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndungulile akimsalimia mmoja wa watoto waliojitokeza kupima afya zao wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani ambapo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni iliyopo wilaya ya Kigamboni. Jumla ya watoto 34 walipima afya zao ambapo sita kati yao walikutwa na matatizo na kupewa rufaa ya kwenda kupata matibabu ya kibingwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete.

Daktari wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Smitha Bhalia akitoa maelekezo ya jinsi ya kutumia dawa kwa mkazi wa Kigamboni  wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani ambapo Taasisi hiyo  kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni iliyopo wilaya ya Kigamboni. Katika upimaji huo makampuni mbalimbali ya dawa za binadamu yaligawa dawa bure kwa watu waliokutwa na matatizo yaliyohitaji kutumia dawa.

Afisa Muuguzi Msaidizi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Irene Isaack akimsajili mkazi wa Kigamboni aliyejitokeza kupima magonjwa ya  moyo pamoja na kupata elimu ya afya bora ya moyo wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani yaliyofanyika hivi karibuni (29/9/2018) ambapo Taasisi hiyo  kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni iliyopo wilaya ya Kigamboni. 

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Ziada Juma akimpima sukari kwenye damu mkazi wa Kigamboni wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani yaliyofanyika hivi karibuni (29/9/2018) ambapo Taasisi hiyo  kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni iliyopo wilaya ya Kigamboni. 

Afisa Lishe wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Maria Semlongo akitoa elimu ya lishe bora kwa afya ya moyo kwa mkazi  wa Kigamboni wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani ambapo Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni iliyopo wilaya ya Kigamboni. Katika upimaji huo makampuni mbalimbali ya dawa za binadamu yalitoa dawa bure kwa wagonjwa waliokutwa na matatizo yaliyohitaji kutumia dawa.

Daktari wa Hospitali ya Vijibweni Edesio Henry akimpatia fomu ya matibabu mkazi  wa Kigamboni Arafa Mohamed wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani yaliyofanyika hivi karibuni (29/9/2018) ambapo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji bila malipo katika viwanja vya Hospitali hiyo  iliyopo wilaya ya Kigamboni.

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Marcerina Granima akitoa elimu ya mazoezi, afya ya moyo na lishe bora kwa wakazi wa Kigamboni wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani ambapo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni   iliyopo wilaya ya Kigamboni. Jumla ya watu 300 walipimwa afya zao ambapo 16 walikutwa na matatizo ya moyo ambayo yalihitaji matibabu ya kibingwa na kupewa rufaa ya kwenda kutibiwa JKCI. 

Afisa Muuguzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Nancy Mallya akimpima shinikizo la damu mkazi wa Kigamboni wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani ambapo Taasisi hiyo  kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni   iliyopo wilaya ya Kigamboni. 

Wafanyakzi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Hospitali ya Vijibweni iliyopo wilaya ya Kigamboni wakimpima mgonjwa kipimo cha kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (ECHO Cardiogram) wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani ambapo Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji wa magonjwa ya moyo bila malipo katika viwanja Hospitali hiyo. Jumla ya wananchi 300 walipima afya zao ambapo 169 wakiwemo watoto  walipimwa kipimo cha ECHO na 135 ambao ni watu wazima walipima kipimo cha kuangalia umeme wa moyo jinsi unavyofanya kazi (Electrocardiography-ECG).

Watoto wakimimwa uzito wakati wa maadhimisho ya siku ya Moyo Duniani ambapo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JCKI)  kwa kushirikiana na Chama cha Madaktari wa Moyo Tanzania (THF) walifanya upimaji wa magonjwa ya moyo bila malipo katika viwanja vya Hospitali ya Vijibweni iliyopo wilaya ya Kigamboni.

Comments

Popular posts from this blog

JKCI yawafanyia upasuaji wa Moyo wagonjwa 36 bila kufungua kifua

Balozi wa Uholanzi nchini Mhe. Jeroen Verheul aipongeza Taasisi ya Moyo Nchini

Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na wenzao wa Shirika la Balsam Care & Care la nchini Saudi Arabia wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo bila kufungua kifua

JKCI Kutambulika Kimataifa kwa Kazi Bora za Upasuaji wa Moyo